Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 2 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 29 2019-11-06

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA aliuliza:-

Shirika la Mzinga limekuwa likifanya kazi zake kwa weledi na uaminifu mkubwa lakini lina changamoto za vifaa kama vile mashine za ramani:-

Je, kwa mwaka 2019/2020 Serikali ilitenga kiasi gani cha fedha kwa ajili ya Shirika hilo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maryam Salum Msabaha, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2019/2020, Shirika la Mzinga limetengewa jumla ya shilingi 2,000,000,000.00 kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuhakikisha shirika linatekeleza majukumu yake kwa ufanisi, shirika limeanza kutekeleza Mpango Mkakati wa Miaka Mitano (2017/2018 – 2021/2022) ambao unakusudia kupanua wigo wa uzalishaji wa mazao ya kijeshi. Aidha, shirika limepanga kuanzisha kiwanda cha kutengeneza baruti kwa ajili ya matumizi yasiyo ya kivita (civil explosives) na kupanua mradi wa kutengeneza mashine ndogo ndogo zitakazowezesha wajasiriamali kuongeza thamani ya mazao ya kilimo na misitu.