Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 17 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 13 2019-11-05

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA (K.n.y. MHE. DEO K. SANGA) aliuliza:-

Askari wa Kituo cha Polisi katika Mji wa Makambako hawana gari la doria wala nyumba za kuishi:-

(a) Je, ni lini Serikali itajenga nyumba za kuishi Askari hao?

(b) Je, ni lini Serikali itatoa gari la doria kwa Kituo cha Polisi Makambako?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Makambako ina askari wapatao 111 na kuna jumla ya nyumba 12 tu katika Mji wa Makambako. Nyumba hizo ni takribani asilimia 11 ya mahitaji halisi ya nyumba za makazi na askari katika mji huo. Hata hivyo, katika jitahada za kutatua changamoto hiyo, mwezi Oktoba, 2018 Serikali imeanzisha ujenzi wa nyumba 20 katika Mji wa Makambako ambapo nyumba hizi kwa sasa zimeshakamilika na askari wameshahamia.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Makambako kwa sasa ina magari matatu; magari mawili ya zamani ambapo moja ni PT. 0766 Landrover inayohitaji matengezo makubwa ili liweze kufanya kazi; na nyingine ni aina ya PT.1912 Toyota Land Cruiser ambayo ndiyo inatumika ingawa inafanyiwa matengenezo ya hapa na pale. Gari hili ndiyo inalotumika kwenye doria na operesheni mbalimbali pamoja na kupeleka askari kwenye matukio makubwa yanayotokea sehemu za mbali. Doria katika Mji wa Makambako hufanyika kwa kutumia gari, miguu pamoja pikipiki.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, mwezi Septemba mwaka 2018 Wilaya ya Makambako imepata mgao wa gari jipya moja aina ya Ashok Leyland kwa ajili ya kusaidia utekelezaji wa shughuli mbalimbali za Jeshi la Polisi katika wilaya hiyo. (Makofi)