Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 107 2020-02-07

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE M. LUBELEJE aliuliza:-

Kati ya Kijiji cha Mbori na Kijiji cha Tambi upo mto ambao hujaa maji wakati wa mvua na kusababisha wananchi na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Tambi na Sekondari ya Matomondo kushindwa kuvuka:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja katika mto huo ili wananchi na wanafunzi waweze kuvuka?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa George Malima Lubeleje, Mbunge wa Mpwapwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umepanga katika mwaka wa fedha 2019/2020 kufanya usanifu kwa ajili ya ujenzi wa daraja linalounganisha Vijiji vya Mbori na Tambi vilivyopo katika Wilaya ya Mpwapwa ili kurahisisha mawasiliano kati ya maeneo hayo. Kazi hiyo ya usanifu itakapokamilika itawezesha kujua gharama zinazohitajika ili kutafuta fedha za kuanza ujenzi wa daraja hilo.