Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 90 2020-02-05

Name

Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS) aliuliza:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kufunga Kamera ndani ya Vituo vya Polisi sasa ili kupunguza malalamiko kwa baadhi ya wananchi wanapohudumiwa kwa kumwezesha Mkuu wa Kituo kufuatilia mwenendo wa shughuli za Kituo akiwa Ofisini au kwa kutunza kumbukumbu za matukio yanayotokea kwenye vituo hivyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tauhida Cassian Gallos, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, suala la matumizi ya CCTV Camera katika vituo vyetu ni la umuhimu mkubwa katika kuhakikisha huduma ya Polisi kwa wananchi zinatolewa kwa weledi na kwa kuzingatia maadili ya Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Spika, Jeshi la Polisi lina nia ya kufanya maboresho yakiwemo matumizi ya TEHAMA kwa kufunga kamera katika vituo vyake ili kuwapa nafasi Viongozi wa Kamandi kufuatilia matukio mbalimbali yanayotokea vituoni ikiwemo namna Askari wa chini wanavyohudumia wananchi.

Aidha, kutokana na ufinyu wa bajeti unaochangiwa na wingi wa changamoto, Jeshi la Polisi kwa sasa halina bajeti hiyo. Hata hivyo, limeruhusu wadau katika maeneo mbalimbali kuwezesha ufungaji wa kamera za ufuatiliaji kwa nia ya kuboresha na kufuatilia utendaji wa Askari.

Mheshimiwa Spika, napenda kutumia nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge kushirikisha wadau katika maeneo yao kuchangia upatikanaji na ufungaji wa CCTV Camera vituoni ili kupunguza malalamiko ya huduma isiyo na weledi ya Askari kwa wananchi.