Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 83 2020-02-05

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-

Watu wanaoishi na VVU wanapata shida sana katika kupata lishe bora na matibabu ya uhakika:-

(a) Je, Serikali imejipangaje katika kuwapa mikopo itakayowasaidia kuendesha maisha yao kupitia vikundi mbalimbali?

(b) Je, kwa nini Serikali isione umuhimu wa kutenga sehemu ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya kundi hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Wingwi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Serikali inatoa dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI kwa wagonjwa wote wanaoishi na VVU ili kuimarisha afya zao na kuwakinga na magonjwa nyemelezi. Aidha, kwa kuwa watu wanaoishi na VVU wanashiriki kama kawaida katika shughuli za ujenzi wa Taifa, Serikali inawanashauri waendelee kutumia fursa za mikopo zinazotolewa na taasisi za kifedha ikiwemo pamoja na Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) na VICOBA.

Mheshimiwa Spika, Serikali inashauri na kusisitiza watu wanaoishi na VVU kuitumia fursa ya mikopo inayotolewa kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi na jumuishi yatakayonufaisha makundi yote kiuchumi wakiwemo watu wanaoishi na VVU.