Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 81 2020-02-05

Name

Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL aliuliza:-

Halmashauri ya Manispaa ya Moshi haina Hospitali ya Wilaya na kuifanya Hospitali ya Mkoa ya Mawenzi izidiwe na idadi ya wagonjwa:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha ili kujenga Hospitali ya Wilaya katika Manispaa ya Moshi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Raphael Japhary Michael, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inakamilisha taratibu za kukabidhi majengo na ardhi ya Kituo cha Afya Moshi Arusha kwa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ili kipanuliwe na kupandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Halmashauri. Baada ya kukamilika kwa taratibu hizo, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu inayohitajika kwa hadhi ya Hospitali ya Halmashauri.

Mheshimiwa Spika, aidha, kwa sasa wananchi wa Manispaa ya Moshi wanapata huduma katika Hospitali Teule ya Mtakatifu Joseph ambayo inafuata miongozo ya Serikali kwa kutoa matibabu bure kwa wazee, watoto chini ya miaka mitano na akina mama wajawazito.