Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 43 2019-09-06

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, ni lini Halmashauri ya Mji wa Mafinga itaingia katika mpango wa uendelezaji na uboreshaji wa Miji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Fedha na Mipango na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) iliingia makubaliano ya mkopo wa masharti nafuu kwa ajili ya kuendeleza na kuboresha miji nchini. Programu hii ina maeneo mawili katika uboreshaji; uboreshaji wa miundombinu na kuzijengea uwezo Halmashauri hizi ili ziweze kufanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya vigezo vilivyokuwa vimewekwa katika programu hii ni kuwa, ili Halmashauri iweze kuingia katika utekelezaji wa programu ni lazima iwe Manispaa au Mji. Hivyo, Mafinga ilikosa sifa za kuwa katika programu hii kwa wakati huo, ambapo ilianza kutekelezwa mwaka 2012, bado Mafianga haikuwa na hadhi ya Mji. Utekelezaji wa programu hii ulipaswa kukamilika Desemba, 2018. Hata hivyo, kutokana na changamoto mbalimbali programu hii imeongezewa muda hadi Juni, 2020.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika utekelezaji wa programu hii, Serikali imeanza mazangumzo na Benki ya Dunia ili kuwa na programu nyingine ya uboreshaji na uendeshaji wa miji nchini itakayoanza baada ya kwisha kwa programu hii ya sasa. Serikali itatoa kipaumbele kwa Miji na Manispaa ambayo haikuwepo kwenye programu awamu ya kwanza ikiwemo Mafinga Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.