Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 75 2020-02-04

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE (K.n.y MHE. KABWE Z. R. ZITTO) aliuliza:-

Watanzania wanaoishi nje ya nchi wanapata changamoto za huduma za uhamiaji kutokana na Balozi zetu takribani zote kutokuwa na Maafisa Uhamiaji.

Je, ni lini Serikali itapeleka Maafisa Uhamiaji kuhudumu kwenye Balozi zetu ili kutoa huduma bora kwa raia wa Tanzania kwenye nchi hizo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Uhamiaji inawajibika kuhakikisha Watanzania wanaoishi nje ya nchi wanapata huduma bora za uhamiaji wanapofika kwenye Balozi zetu nje ya nchi. Maafisa Uhamiaji waliokuwa wanatoa huduma za uhamiaji katika Balozi zetu ama wamestaafu au wamemaliza muda wao wa kuhudumu katika Balozi walizokuwa na wamerejea nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuhakikisha huduma bora za uhamiaji zinaendelea kutolewa kwa raia wa Tanzania wanaoishi nje ya nchi, tayari Serikali imewateua maafisa watano kutoka Idara ya uhamiaji ambao wamepatiwa mafunzo ya kuhudumu katika Balozi. Kwa sasa Idara ya Uhamiaji kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wako katika hatua za mwisho za kukamilisha taratibu za kuwapeleka Maafisa hao kwenda kuhudumu katika Balozi walizopangiwa.