Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 44 2020-01-31

Name

Susanne Peter Maselle

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSANNE P. MASELLE aliuliza:-

Bado kuna shida kubwa ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wetu hasa maeneo ya vijijini:-

Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu kupunguza au kumaliza tatizo hilo kwa wananchi wa maeneo mbalimbali ya Misungwi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Susanne Peter Maselle, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto ya maji kwa wananchi wa maeneo mbalimbali ya Misungwi, Serikali imekamilisha ujenzi wa mradi wa maji wa thamani ya shilingi bilioni 12.85 kutoka katika chanzo cha maji cha Nyahiti ambapo wakazi wapato 64,280 wanatarajia kunufaika katika mradi huo hadi kufikia mwaka 2040.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mradi huo, Serikali inatekeleza mradi mkubwa kutoka bomba kuu la usafirishaji maji la KASHWASA utakaohudumia vijiji 14 vya Wilaya ya Misungwi kupitia miradi mitano. Mradi wa kwanza ni kufikisha huduma ya maji Mabale – Mbarika, mradi wa pili ni kufikisha huduma ya maji Igenge, mradi wa tatu ni kufikisha huduma ya maji Mbarika – Ngaya, Mradi wa nne ni kufikisha huduma ya maji Ngaya – Matale na mradi wa tano ni kufikisha huduma ya maji Matale – Misasi. Miradi hii ikikamilka itahudumia jumla ya watu 45,788.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imeanza kutekeleza miradi katika vijiji vitano vya Kata ya Shilalo kupitia Programu ya Malipo kwa Matokeo, inayofadhiliwa na Benki ya Dunia. Miradi hiyo ikikamilika itahudumia watu wapatao 15,500. (Makofi)