Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 35 2020-01-30

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SABREENA H. SUNGURA aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza mahabusu katika Magereza na Vituo vya Polisi nchini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sabreena Hamza Sungura, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kipindi hiki kirefu Serikali kupitia vyombo vyake vya haki jinai nchini imekuwa ikifanya juhudi mahususi kupunguza idadi ya mahabusu katika Magereza yote hapa nchini. Kupitia mikakati mbalimbali idadi ya mahabusu imekuwa ikipungua mara kwa mara na bado juhudi zinaendelea za kuhakikisha Magereza yetu yanahifadhi wahalifu kulingana na uwezo wake kisheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya mikakati inayotumika kutatua tatizo la mahabusu Magerezani ni pamoja na Vikao vya Kamati za Kusukuma Kesi (Case Flow Management Committee), Idara ya Mahakama kusisitiza matumizi ya Sheria ya Dhamana kwa makosa yanayodhaminika, uundwaji wa kikosi kazi cha haki jinai kupitia makosa mbalimbali (Criminal Justice System Task Force) pamoja na mikakati mingine inayotokana na Idara ya Mahakama.