Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 18 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 17 2020-01-29

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa Gridi ya Taifa Mkoani Katavi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri na Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dada yangu Anna Richard Lupembe Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) inatekeleza Miradi mbalimbali ya kusafirisha umeme itakayohakikisha kuwa Mikoa yote nchini inaunganishwa katika gridi ya Taifa ikiwemo Mkoa wa Katavi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa sasa kupitia shirika la umeme nchini (TANESCO) inatekeleza Mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Katavi kupitia Ipole na Inyonga yenye urefu wa kilomita 381 ili kuunganisha Mkoa wa Katavi katika gridi ya Taifa. Kazi hiyo pia itahusisha ujenzi wa vituo vya kupoza umeme wa msongo wa kilovoti 132/33 vya Ipole, Inyonga na Mpanda Mkoani Katavi. Gharama za mradi huu ni Shilingi bilioni 135.3.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tarehe 11 Oktoba, 2019 Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huu katika eneo la Orio Mjini Mpanda. Kazi zinazoendelea kwa sasa ni ujenzi wa vituo vya kupoza umeme vya Mpanda, Ipole na Inyonga pamoja na upimaji wa njia ya kusafirisha umeme kwa ajili ya tathmini ya mali za wananchi watakaopisha mradi. Kazi za ujenzi wa mradi huu zinatekelezwa kwa kutumia wataalam wa TANESCO kupitia kampuni tanzu ya ETDCO. Mradi huu unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Mei, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali pia imeanza kutekeleza Mradi mkubwa wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kV 400, Iringa - Mbeya – Tunduma - Sumbawanga – Mpanda - Kigoma – Nyakanazi (North West Grid) yenye urefu wa kilomita 1,384. Mradi huu upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji. Shughuli za ujenzi wa mradi huu zitaanza mwezi Mei, 2020 na zinatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.