Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Madini 11 2019-09-03

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA aliuliza:-

Katika Jimbo la Ngara wapo wachimbaji wadogo wa madini ya Manganese katika Kata ya Murusagamba, Kijiji cha Magamba na tayari wamepata soko la madini hayo nje ya nchi ikiwemo India, Afrika Kusini na Uturuki:-

Je, Serikal iko tayari kutoa kibali kwa wachimbaji hao kuuza madini hayo yakiwa ghafi kutokana na kwamba hakuna mitambo ya uchenguaji hapa nchini?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alex Raphael Gashaza, Mbunge wa Ngara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imendelea kusimamia Sekta ya Madini kikamilifu kwa kuhakikisha shughuli za uchimbaji na biashara ya madini zinafanyika kwa kufuata sheria na taratibu za nchi ili rasilimali hiyo iweze kutoa mchango kwa Serikali kupitia malipo ya tozo stahiki za madini na pia itoe fursa ya ajira kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kutambua umuhimu wa Sekta ya Madini na kwa kuwa rasilimali hiyo siyo jadidifu (non renewable), mwaka 2017 ilifanya marekebisho ya Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na kutunga sheria mpya ya Mali na Urithi wa Asili (The Natural Wealth and Resources (Permanent Sovereignty) Act, 2017) ambayo imerasimisha umiliki wa rasilimali madini kwa Taifa. Kupitia sheria hizo, Serikali imetoa zuio la usafirishaji wa madini ghafi pamoja na makinikia nje ya nchi ili kuhamasisha uwekezaji katika tasnia ya uchenjuaji na uongezaji thamani wa madini nchini ambayo itatoa fursa ya ajira kwa Watanzaia na pia kutekeleza dhima ya Serikali ya kuwa na uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia changamoto inayowakabili wachimbaji wadogo wa madini ya viwandani yakiwemo madini ya manganese, Serikali inakamilisha utaratibu unaotumika katika kipindi cha mpito hasa kwa wachimbaji wadogo waliokuwa wamezalisha madini yao na kulipia tozo zote za Serikali kabla ya zuio hilo.