Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 10 2019-09-03

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND aliuliza:-

Afya za wanawake wengi vijijini zinaathiriwa na moshi wa kuni wanazopikia kwenye majiko ya mafiga matatu ambayo yanatumia kuni nyingi na hivyo kuchochea kasi ya ukataji miti:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa matumizi ya majiko ya mafiga matatu kote nchini?

(b) Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuondoa majiko hayo kwenye shule zote za msingi na sekondari?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shally Josepha Raymond, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, matumizi ya tungamotaka hususan kuni na mkaa kama chanzo cha nishati ya kupikia hapa nchini yanakadiriwa kufikia asilimia 85. Matumizi ya tungamotaka ikiwemo mafiga matatu husababisha madhara ya kiafya kutokana na kuvuta hewa chafu inayotokana na kuni na mkaa kwa watumiaji pamoja na uharibifu wa mazingira kutokana na ukataji wa miti.

Mheshimiwa Spika, kupitia Sera ya Taifa ya Nishati ya mwaka 2015, Serikali imekuwa ikihamasisha matumizi bora ya nishati ikiwemo teknolojia zinazopunguza gesi ya ukaa na matumizi makubwa ya kuni na mkaa kwa kutumia majiko banifu. Aidha, Serikali imekuwa ikihamasisha kuacha matumizi ya nishati mbadala wa kuni na mkaa katika kupikia gesi na mitungi (Liquefied Petroleum Gas), bayogesi, vitofali vya mabaki ya tundamotaka na majiko ya nishati jua.

Mheshimiwa Spika, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kupitia Mfuko wa Nishati Vijijini pamoja na jukumu la kusambaza umeme vijijini inasaidia usambazaji wa teknolojia bora za kupikia hususan katika taasisi za Umma nchi nzima zikiwemo Shule, Magereza, Kambi za Wakimbizi na Zahanati.