Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 30 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 251 2019-05-17

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza:-

Mgogoro wa ardhi kati ya Jeshi la magereza na wananchi wa Kata ya Ukondamayo hususan Kijiji cha Tumaini umedumu kwa muda mrefu sasa.

Je, Serikali inachukua hatua gani kutatua na kumaliza mgogoro huu?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Margaret Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kukujulisha kwambakwa sasa hakuna mgogoro wa ardhi kati ya kata ya Ukandamoyo hususani kijiji cha Tumaini na gereza la ilimo Urambo. Ni kweli hapo awali ulikuwepo mgogoro baina vya vijiji vinne mojawapo kijiji cha tumaini, Mgogoro huo ulitatuliwa na kuhitishwa mwaka 200 kwa kuhutimishwa mwaka 2000 kwa kushirikishwa viongozi kutoka wizira ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Ardhi, Jeshi la Magereza, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Tabora, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Urambo na Serikali ya vijiij vyote nine vilivyokuwa na mgogoro kikiwemo Kijiji cha Tumaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hitimisho la mgogoro huo ni baada ya Jeshi la magereza kukubali kuotka eneo la jumla ya ekari 3,218 kwa vijiji vilivyokuwa na mgogoro mojawapo kijiji cha Tumaini wakapewa ekari 505, Imalamakoye ekari 195, Nsendakanoge ekari 1,655 na Itebulanda ekari 860.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha hati ya makubaliano ya hitimisho la mgogoro ilisainiwa na viongozi wa vijiji vyote vinne vilivyokuwa na mgogoro kikiwemo kijiji cha Tumaini na mawe ya mipaka yaani beacons yakawekwa upya kwa utambulisho wa namba Uv 66, Uv 69, Uv 107, Uv 35 na Uv 108.