Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 29 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 239 2019-05-16

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA (K.n.y MHE. SABREENA H. SUNGURA) aliuliza:-

Kituo cha Afya Ujiji kinahudumia zaidi ya wakazi 20,000 lakini kituo hicho hakina mashine ya ultrasound.

Je, ni lini Serikali itapeleka mashine ya ultrasound katika kituo hicho?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sabreena Sungura, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/19, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma/Ujiji imeidhinisha kiasi cha Shilingi 15,475,254.28 kupitia Mradi wa Malipo kwa Ufanisi (Result Based Financing) kwa ajili ya ukarabati wa chumba kitakachotumika kwa huduma za mionzi na shilingi 45,000,000.00 zimetengwa kwa ajili ya ununuzi wa ultrasound. Fedha hizo zimepelekwa MSD kwa ajili ya taratibu za ununuzi wa kifaa hicho. Kwa sasa huduma ya Ultrasound inapatikana katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Maweni na Hospitali Teule ya Manispaa ya Baptist.