Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 28 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 238 2019-05-15

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:-

Je, nini mpango wa Serikali juu ya kuboresha jengo la Mahakama Wilayani Nachingwea?

Name

Dr. Augustine Philip Mahiga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mahakama ya Tanzania haipo katika mpango wa maboresho ya majengo ya Mahakama nchini, ambapo pamoja na mambo mengine imekusudia kusogeza haduma ya Mahakama karibu na wananchi. Ili kufikia lengo hilo, Mahakama imeendelea kutatua changamoto kubwa ya uhaba na uchakavu wa majengo kwa kuendelea na kukarabati majengo nchi nzima.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Mahakama ya Tanzania inafahamu tatizo la uchakavu wa majengo mengi ya Mahakama nchini, ikiwemo jengo la Mahakama ya Wilaya Nachingwea. Katika kukabiliana na changamoto hii, Mahakama imeweka kipaumbele katika kuboresha na kujenga majengo ya Mahakama nchini kulingana na mpango mkakati wa miaka mitano ambao umeendelea kutekelezwa kwa awamu kutegemea na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge wa Nachingwea kuwa kutokana na uhitaji mkubwa wa rasilimali na rasilimali chache zilizopo, katika mpango mkakati wa miaka mitano, Mahakama iliamua kujipanga upya na kuweka vipaumbele ili kuhakikisha tunaondokana na changamoto hii. Aidha, tayari tathmini ya jengo la Mahakama Nachingwea imeshafanyika. Kimsingi jengo hili linahitaji kujengwa upya na siyo kufanyiwa maboresho. Aidha, baada ya tathmini hiyo kufanyika ujenzi wa jengo hilo umewekwa kwenye mpango wetu wa ujenzi wa Mahakama wa mwaka 2020/2021kutegemeana na upatikanaji wa fedha.