Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 28 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 235 2019-05-15

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM aliuliza:-

Kumekuwa na malalamiko ya muda mrefu ya wananchi ambao maeneo yao yametwaliwa na Jeshi la Wananchi (JWTZ) pasipo kulipwa fidia:-

Je, Serikali ina mpango gani wa haraka kulipa fidia kwa wannachi hao?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masoud Abdalah Salim, Mbunge wa Ntambile, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika ni kweli yapo maeneo mbalimbali yaliyotwaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania kwa ajili ya utekelezaji wa jukumu la ulinzi wa nchi na mipaka yake. Baadhi ya maeneo hayo yamelipwa fidia na mengine mchakato wa kulipa fidia kwa wamiliki unaendelea.

Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali uliopo ni kuendelea na utaratibu wa kulipa fidia stahiki kwa wananchi kadri hali ya fedha itakavyoruhusu na kwa mujibu wa Sheria ya Utwaaji Ardhi kwa ajili ya matumizi ya umma. Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Wizara ilitenga shilingi bilioni 20.9 kwa ajili ya kulipa fidia maeneo yaliyotwaliwa na jeshi. Baada ya uhakiki wa malipo ya fidia tayari kiasi cha shilingi bilioni 3 kimelipwa kama fidia. Aidha, uhakiki wa madai ya fidia unaendelea katika maeneo mengine na mara uhakiki utakapokamilika Serikali kupitia Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa italipa fidia hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba wananchi wawe na subira wakati Serikali inakamilisha uhakiki ili kuwalipa stahiki zao.