Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 27 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 229 2019-05-14

Name

Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. MAULID S. A. MTULIA aliuliza:-

Vijana wetu wanafanya kazi za sanaa nzuri sana lakini kipato wanachokipata hakilingani na ubora wa kazi zao:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwasaidia vijana hawa kupata stahiki ya kazi zao?

(b) Je, sera na sheria zinasaidiaje wasanii wetu kumiliki na kunufaika na kazi zao za sanaa?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Said Mtulia, Mbunge wa Kinondoni, lenye sehemu (a) na (b), kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Utamaduni ya Mwaka 1997 inaelekeza kuanzishwa kwa chombo cha kusimamia hakimiliki ambayo ni sehemu muhimu ya dhana pana ya haki bunifu (intellectual property). Hivyo, mwaka 1999 ikatungwa Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki ambayo chini yake maslahi ya watunzi wa kazi za Sanaa, watafsiri, watayarishaji wa kuhifadhi sauti, wachapishaji na kadhalika yanalindwa kisheria na chombo cha kusimamia haki hizo, yaani Chombo cha Hakishiriki Tanzania (COSOTA).