Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 219 2019-05-13

Name

Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA (K.n.y. MHE. AGNESS M. MARWA) aliuliza:-

Nyumba nyingi za Vijijini hazikuwekewa umeme wakati wa usambazaji japo baada ya kuweka umeme kumekuwa na ongezeko la ujenzi wa nyumba na uzalishaji mali kama ujasiriamali.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha nyumba zote zilizobaki zinapata umeme kabla mradi wa REA haujamaliza muda wake?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Mathew Marwa Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, lengo la Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ni kupeleka umeme katika Vijiji vyote Tanzania Bara ifikapo Juni, 2021. Ili kutekeleza azma hiyo, Serikali imeweka kipaumbele kwa kusambaza miundombinu ya umeme katika maeneo ambayo hayajafikiwa na miundombinu ya umeme na katika Taasisi zinazotoa huduma za kijamiii kama vile Shule, Zahanati, Makanisa, Misikiti, Vituo vya Afya, Nyumba za Makazi na Biashara na Miradi ya Maji. Utekelezaji wa Mradi wa REA Awamu ya III mzunguko wa kwanza ulianza kutekelezwa mwezi Julai, 2018 na unaendelea katika maeneo yote nchini ambapo utekelezaji wake utakamilika ifikapo mwezi Juni, 2019. Maeneo yatakayobaki ikiwa ni pamoja na nyumba za makazi, Taasisi, miradi ya maji na biashara yatapelekewa umeme kupitia mradi wa REA III Mzunguko wa pili utakaoanza kutekelezwa mwezi Julai, 2019 na kukamilika mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mpango huo, Serikali imebuni miradi ya ujazilizi (Densification) kwa lengo la kujaziliza katika mapungufu kwa miradi iliyotangulia. Miradi hii ya ujazilizi inalenga hasa kuhakikisha nyumba zote katika kila Kijiji na Kitongoji zinaendelea kupata umeme. Shirika la Umeme nchini (TANESCO) nalo linaendelea kusambaza na kuunganisha wateja mara kwa baada ya miradi ya REA kukamilika. Ili kuhakikisha wananchi wote wa Vijijini wanaunganishiwa umeme kwa gharama nafuu ya shilingi 27,000, ahsante sana.