Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 218 2019-05-13

Name

Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARY D. MURO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia Wananchi wa Kiluvya, Madukani, Mwanalugali na Mikongeni ambao wamepisha ujenzi wa njia ya umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mary Deo Muro, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza mradi wa kujenga njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovot 400 kutoka Kinyerezi (Dar es Salaam) na Rufiji (Pwani) kupitia Chalinze hadi Dodoma kupitia maeneo ya Kiluvya, Madukani na Mwanalugali. Mradi huu unalenga kuongeza upatikanaji wa umeme katika ukanda wa Mashariki, Kati na Kaskazini mwa nchi kutoka katika mitambo ya kuzalisha umeme ya Kinyerezi na mradi wa Rufiji.

Mheshimiwa Spika, upimaji wa njia na uthamini wa mali za wananchi watakaopisha mradi ulikamilika mwaka 2018. Jumla ya shilingi bilioni 21 na milioni 600 zinatakiwa kulipwa kama fidia kwa wananchi katika maeneo ya Halmashauri za Kisarawe, Kibaha Mjini na Kibaha Vijijini ikiwemo wananchi wa Vijiji vya Chalinze, Kiluvya madukani na Mwanalugali. Katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali imetenga fedha shilingi bilioni 50 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi wa maeneo hayo baada ya kukamilisha uhakiki wa madai hayo.


Mheshimiwa Spika, Serikali inawaomba wananchi wavute subira wakati Serikali inaendelea kukamilisha taratibu za malipo haya, ahsante sana.