Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 26 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 217 2019-05-13

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASHA MSHIMBA JECHA (K.n.y. MHE. ASHA ABDULLAH JUMA) aliuliza:-

Je, Serikali inachukua hatua gani kuwasadia wananchi walioweka amana zao katika Benki ya FBME.

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Asha Abdullah Juma, Mbunge Vitib Maalumu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Mabenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006 kifungu cha 39(2) na (3), amana au akiba za wateja katika benki au taasisi ya fedha, zina kinga ya bima ya amana ya kiasi kisichozidi shilingi za kitanzania 1,500,000 tu. Endapo mteja hana salio la amana la kiasi kilichozidi shilingi 1,500,000 atapata fidia ya asilimia 100.

Mheshimiwa Spika, wateja walio na amana zaidi ya shilingi 1,500,000, wanalipwa shilingi 1,500,000 kama fidia ya bima ya amana, na kiasi kinachobakia kinalipwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za ufirisi. Aidha malipo kwa mujibu wa sheria na taratibu za ufirisi yanategemea makusanyo ya fedha kutoka kwenye mauzo ya mali pamoja na fedha zilizowekezwa na benki katika taasisi mbalimbali za fedha za ndani na nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, zoezi la kukusanya mali na fedha zilizokuwa zimewekezwa na za benki ya FBME katika taasisi mbalimbali za fedha, hususan nje ya nchi, limekumbwa na changamoto za kisheria kati ya Tanzania na nchi ya Cyprus ambako benki ya FBME ilikuwa na tawi lililokuwa linaendesha sehemu kubwa ya biashara zake, na hivyo kusababisha ucheleweshaji wa ukusanyaji na ugawaji wa fedha za ufilisi. Hivyo basi tarehe ya kuanza kulipa fedha zinazotokana na ufilisi haijulikani kwa sasa kutokana na uwepo wa kesi zinazokwamisha zoezi la ukusanyaji mali na madeni ya benki ya FBME. Serikali kupitia Bodi ya Bima ya Amana, Benki Kuu ya Tanzania pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ipo katika mazungumzo na Serikali ya Cyprus ili kulipatia suala hili ufumbuzi.