Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 206 2019-05-10

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DANIEL E. MTUKA aliuliza:-

Kumekuwa na ajali za barabarani za kutisha katika Milima ya Sukamahela eneo la Mbwasa, Manyoni na Sekenke Shelui:-

(a) Je kwa kipindi cha miaka miwili yaani 2016 na 2017, ni ajali ngapi zimetokea katika milima tajwa?

(b) Je, ni watu wangapi wamepoteza maisha na wangapi walijeruhiwa katika kipindi hicho?

(c) Je, Serikali inatoa tamko gani ili kupunguza au kukomesha kabisa ajali katika maeneo haya ndani ya Mkoa wa Singida?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Edward Mtuka, Mbunge wa Manyoni Mashariki, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya ajali 28 zimetokea katika kipindi cha miaka miwili yaani tarehe 1 Januari, 2016 mpaka tarehe 31 Disemba, 2017 katika sehemu hiyo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameitaja.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, jumla ya watu 33 wamepoteza maisha na jumla ya watu 26 walijeruhiwa katika kipindi tajwa.

(c) Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inawataka madereva kuwa makini wanapoendesha vyombo vya moto barabarani na wazingatie sharia, kanuni, taratibu na alama na michoro ya barabarani. Pia waendeshe kwa kuzingatia udereva wa kujihami (defensive driving) ili kuepusha ajali, kwani ajali nyingi zinazotokea katika maeneo haya zinasababishwa na uzembe wa madereva, ubovu wa magari, uchovu wa madereva hususani kwenye uwepo wa kona kali, milima na miteremko mikali.