Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 23 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 188 2019-05-08

Name

Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Primary Question

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE aliuliza:-

Kuna uhaba mkubwa wa Walimu wa Shule za Msingi Wilayani Mwanga:-

Je, ni lini Serikali itapeleka Walimu 384 wanaohitajika?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Jumanne Abdallah Maghembe, Mbunge wa Mwanga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna changamoto ya upungufu wa walimu wa shule za msingi nchini, na Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga ina jumla ya shule za msingi 110, za Serikali zenye jumla ya walimu 590, hadi kufikia Novemba, 2018 kulikuwa na upungufu wa walimu 384.

Mheshimiwa Spika, Mwezi Aprili, mwaka 2019, Serikali imeajiri walimu 4,549 wa shule za msingi na sekondari ili kuziba nafasi zilizoachwa wazi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Halmashauri ya Mwanga, na kati ya walimu hao 3,089 ni kwa shule za msingi na walimu1,460 ni shule za sekondari. Walimu hawa wameshapangwa katika halmashauri mbalimbali nchini na walipaswa kulipoti kuanzia jana mpaka tarehe 21 na wale ambao hawataripoti, nafasi zao zitapewa watu wengine ambao wana uhitaji kama huo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, halmashauri ya Mwanga imepelekewa walimu 21 wa shule za msingi nawalimu watano wa shule za sekondari. Serikali itaendelea kuajiri walimu kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, ahsante.