Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 22 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 183 2019-05-07

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:-

Jimbo la Kalenga lina vivutio vya utalii vinavyoweza kuingiza nchi yetu pesa za kigeni kama vile Isimila Stone Age na Makumbusho na Mtwa Mkwawa Mkwavinyika:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kushirikiana na Halmashauri ya Iringa Vijijini kuimarisha na kujenga mazingira na kuvitumia vivutio hivyo ili kuongeza Pato la Taifa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Jimbo la Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Isimila Stone Age na Makumbusho ya Mtwa Mkwawa yanasimamiwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambapo Shirika lina jukumu la kuhifadhi na kuendeleza vituo hivi. Aidha, kwa kuzingatia changamoto zilizopo katika vituo tajwa, Wizara kupitia Mradi wa Kusimamia Maliasili na Kuendeleza Utalii, Nyanda za Juu Kusini yaani (Resilient Natural Resources for Tourism and Growth - REGROW) na kwa kushirikiana na Halmashauri za Mkoa wa Iringa, itaimarisha miundombinu hiyo. Kwa kupitia mradi wa REGROW maeneo haya yataboreshwa ikiwa ni pamoja na kujenga ituo cha Kumbukumbu na Taarifa ili uhifadhi Kumbukumbu ya Mtwa Mkwawa na utamaduni wa Wahehe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sanjari na hatua hiyo, Wizara kwa kushirikiana na Mkoa wa Iringa pamoja na Chuo Kikuu cha Iringa imekarabati boma la Mjerumani na kulifanya kuwa Makumbusho ya Mkoa. Aidha, Wizara ilitoa wataalam wa ujenzi kuandaa na kupanga vioneshwa ndani ya makumbusho ya jengo hilo, duka la zawadi, mgahawa na studio ya kurekodi nyimbo za asili. Mapato yatokanayo na jengo hilo yanaingia katika Mkoa wa Iringa.