Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 20 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 158 2019-05-03

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:-

Mafuriko yaliyotokea Mlalo mwaka 1993 yalisababisha uharibifu mkubwa kwa barabara inayounganisha Tarafa za Umba na Mtae:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha za kukarabati barabara hiyo muhimu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Abdallah Shangazi, Mbunge wa Mlalo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara inayounganisha Tarafa za Umba na Mtae yenye urefu wa kilometa 12.7 inajulikana kama barabara ya Mtae – Mtii – Mnazi. TARURA Wilaya ya Lushoto imekamilisha usanifu na tathmini ya kuifanyia matengenezo makubwa, ambapo kiasi cha shilingi bilioni 2.5 kinahitajika.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kugharamia matengenezo hayo kwa kuwa inatambua umuhimu wa barabara hii.