Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 19 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 157 2019-05-02

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:-

Serikali ilianzisha Kanda Maalum ya Kipolisi Dar es Salaam na kufanya Wilaya ya Temeke kuwa Mkoa wa Kipolisi; tangu Temeke iwe Mkoa wa Kipolisi kumekuwa na ongezeko kubwa la uhalifu hasa maeneo ya Jimbo la Mbagala:-

(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kituo cha Mkuu wa Polisi Wilaya ya Mbala?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Vituo vya Polisi na kuviongezea askari, vitendea kazi na kujenga nyumba za askari katika maeneo ya Jimbo la Mbagala?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mbagala ni Wilaya mpya ya Kipolisi iliyopo katika Mkoa wa Kipolisi wa Temeke. Kama ilivyo kwa wilaya nyingine katika Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Wilaya ya Mbagala inahitaji kujengewa Kituo cha Polisi chenye hadhi ya Wilaya. Kwa sasa wananchi wa Mbagala wanahudumiwa katika Kituo cha Polisi cha Mbagala Kizuiani ambacho miundombinu yake haitoshelezi. Aidha, hali kibajeti itakaporuhusu, Serikali itaweka mpango wa kuwajengea wananchi wa Mbagala Kituo kipya cha Polisi, nyumba za makazi ya askari na ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Mbagala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuweza kukabiliana na uhalifu, Wilaya ya Kipolisi Mbagala imepata mgao wa magari matatu (3) aina ya Leyland Ashock Stile yenye Na. PT 3779; PT 3881 na PT 3891 na kufanya jumla ya magari yote katika Wilaya ya Mbagala kuwa tisa ambayo yanatumika kwa shughuli za doria, upelelezi na operesheni mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha usalama katika Wilaya ya Mbagala.