Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 15 | Sitting 17 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 143 | 2019-04-29 |
Name
Ignas Aloyce Malocha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwela
Primary Question
MHE. IGNAS A. MALOCHA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya maandalizi ya awali ya upembuzi yakinifu kwa ajili ya kuweka lami barabara muhimu ya Kibaoni-Kasansa-Muze- Kilyamatundu-Kamsamba kutokea Mlowo; ambayo inaunganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?
Name
Eng. Atashasta Justus Nditiye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kujibiwa swali la Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza kutekeleza mipango ya ujenzi wa barabara ya Kibaoni- Majimoto- Kisansa-Muze-Kilyamatundu- Kamsamba hadi Mlowo yenye urefu wa kilometa 149 kwa kuanza na ujenzi wa daraja la Momba ambalo limekamilika hivi karibuni. Daraja hili limekuwa kikwazo kikubwa cha mawasiliano kati ya wananchi wa Mikoa ya Katavi, Rukwa na Songwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kutambua umuhimu wa barabara hii katika mwaka wa fedha 2018/2019, jumla ya shilingi milioni 200 zilitengwa kwa ajili ya upembuzi yakinifu wa barabara ya Kibaoni-Majimoto-Inyonga ikiwa ni sehemu ya barabara ya Kibaoni-Kasansa-Muze-Kilyamatundu- Kamsamba hadi Mlowo. Aidha, katika mwaka wa fedha 2019/2020, fedha zimeombwa kwa ajili ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Ntendo-Muze- Kilyamatundu ikiwa pia ni sehemu ya barabara ya Kibaoni –Kasansa-Muze-Kilyamatundu-Kamsamba hadi Mlowo. Mara baada ya kukamilika upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na maandalizi ya nyaraka za zabuni za gharama ya ujenzi kujulikana Serikali itatafuta fedha za kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara hii.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved