Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 15 | Sitting 17 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 142 | 2019-04-29 |
Name
Musa Rashid Ntimizi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Igalula
Primary Question
MHE. MUSA R. NTIMIZI alliuliza:-
Kata ya Mmale haina mawasiliano kabisa ya simu:-
Je ni lini Serikali itawapatia wananchi hao mawasiliano kwa kuweka minara ya mawasiliano katika kata hiyo?
Name
Eng. Atashasta Justus Nditiye
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Muhambwe
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Musa Rashid Ntimizi, Mbunge wa Igalula, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Uyui, zaidi ya wakazi 66,056 wamefikishiwa huduma za mawasiliano katika Kata za Kizengi, Loya, Lutende, Mabama na Miswaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na mafanikio hayo, bado kuna changamoto za upatikanaji wa huduma za mawasiliano katika Kata ya Mmale. Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote itaviainisha vijiji vya Kata ya Mmale iliyopo katika Jimbo la Igalula kwa kufanya tathmini ya mahitaji kwa ajili ya kuvifikishia huduma ya mawasiliano na kuvijumuisha katika orodha ya miradi itakayoingia katika zabuni zinazotarajiwa kutangazwa ifikapo mwezi ujao wa tano.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved