Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 16 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 135 2019-04-25

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-

Vitendo vya utekaji kwa watu wasio na hatia na kuwatesa, kuwahujumu na hata kuwaua vinaendelea kukithiri nchini:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzuia, kulinda na kuhakikisha inakomesha vitendo hivyo haraka sana?

(b) Je, hadi sasa ni watu wangapi ambao wamekamatwa na kuchukuliwa hatua kutokana na uhalifu huo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Wingwi, lenye Sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, jukumu la msingi la Serikali ni kuhakikisha raia wake wanakuwa salama wakati wote na wanaendelea na shughuli za uzalishaji mali na shughuli nyingine za kijamii kwa amani na utulivu pasipokuwa na hofu. Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kwenye taarifa za utekaji, utesaji ama mauaji zinapotolewa lengo likiwa ni kuwabaini, kuwachukulia hatua za kisheria watu ambao wanajihusisha na vitendo hivyo.

(b) Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kutumia taarifa za kiitelijensia imekuwa ikiweka mikakati mbalimbali ya kudhibiti mipango ya wahalifu kwa kufanya operesheni na doria mbalimbali kwa lengo la kuzuia na kukomesha vitendo vya aina hii ambapo hadi sasa mtuhumiwa mmoja amekamatwa kwa makosa ya utekaji nyara.