Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 15 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 131 2019-04-24

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itachukua hatua za kimkakati kuhakikisha kwamba migogoro kati ya wafugaji na wananchi wanaoishi pembezoni mwa mbuga za wanyama inakwisha kabisa?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pudenciana Wilfred Kikwembe, Mbunge wa Kavuu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kufuatia kuwepo kwa migogoro mingi baina ya wafugaji na wananchi wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alitoa agizo la kutoviondoa vijiji 396 vilivyoainishwa kuwa na migogoro katika maeneo ya hifadhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Mheshimiwa Rais kutoa agizo hilo kamati maalum iliundwa kwa lengo la kumshauri juu ya namna bora ya kutekeleza agizo hilo. Kamati hiyo iliongozwa na Waziri wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Wizara zingine zilizohusika ilikuwemo Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira, Ofisi ya Maliasili na Utalii, Mifugo na Uvuvi, TAMISEMI, Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Kilimo na Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati imekamilisha utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Rais na maelekezo ya Serikali kuhusu suala hilo yatatolewa na kwa wananchi.