Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 15 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 127 2019-04-24

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:-

Je, ni lini kiwanda cha Saruji cha Dangote kitapewa gesi asilia na TPDC?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petrol Nchini (TPDC) imekamilisha kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kupeleka gesi asilia katika mitambo ya kuzalisha umeme wa muda katika Kiwanda cha Saruji cha Dangote umbali wa mita 100 kutoka katika Toleo la Kwanza la Gesi (Block Valve Station No. 1).

Mheshimiwa Mwenyekiti, awamu ya kwanza ya mradi wa kuwezesha matumizi ya gesi kuzalisha umeme kwa Kiwanda cha Dangote ilikamilika na kuanza kufanya kazi Agosti, 2018 ambapo hadi kufikia Aprili, 2019, Kiwanda cha Dangote kimeanza kutumia wastani wa futi za ujazo milioni tano kwa siku kwa kuzalisha umeme.

Awamu ya pili ya mradi inahusu ujenzi wa miundombinu ya bomba la kusafirisha gesi asilia kutoka BVS 1 kwenda kwenye Kiwanda cha Dangote, umbali wa kilimita 2.7 kwa ajili ya kuwezesha gesi asilia kutumika kama nishati ya kuchoma malighafi ya kuzalisha saruji. Jumla ya gharama za mradi ni shilingi bilioni nane na milioni mia mbili. Awamu ya pili ya mradi ilikamilika Desemba, 2018 na sasa Kiwanda cha Dangote kinatumia gesi ya wastani wa futi za ujazo milioni 15 hadi 20 kwa siku kwa ajili ya uzalishaji wa saruji.