Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 123 2019-04-24

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Madiwani nchini wanafanya kazi kubwa sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaongezea posho na mishahara au maslahi yao?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kazi kubwa wanayofanya Waheshimiwa Madiwani katika kusimamia shughuli za maendeleo kwenye maeneo yao. Kwa kuzingatia ukweli huo, Serikali imekuwa ikipandisha posho na maslahi ya Madiwani kwa kadri mapato ya Halmashauri yanavyoongezeka. Kuanzia mwaka wa fedha 2012/2013, Serikali ilipandisha posho ya Madiwani kupitia Waraka wa mwaka 2012 kutoka shilingi 120,000/= hadi 250,000/= kwa mwezi sawa na ongezeko la asilimia 108.3. Aidha, katika mwaka wa fedha 2014/2015, Serikali ilipandisha tena posho za Madiwani kupitia Waraka wa mwaka 2014 kutoka 250,000 hadi 350,000 kwa mwezi sawa na ongezeko la asilimia 40.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, Serikali inalipa pia posho ya madaraka kwa Wenyeviti wa Kamati kiasi cha shilingi 80,000/= kwa mwezi na posho ya kikao kiasi cha shilingi 40,000/= kwa mujibu wa Waraka wa Mwaka 2007.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kigezo kikubwa kinachotumika kupandisha posho za Madiwani ni uwezo wa Halmashauri kukusanya mapato ya ndani ya Halmashauri husika. Serikali itaendelea kuthamini na kutambua kazi kubwa na nzuri inayotekelezwa na Waheshimiwa Madiwani na kuongeza posho hizo kadri makusanyo ya mapato yanavyoongezeka.