Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 121 2019-04-23

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:-

Serikali ina mpango wa kufikia uzalishaji wa zaidi ya megawatts 5,000 za umeme ifikapo 2020.

Je, ni mkakati gani umewekwa ili kufikia lengo hilo?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zainab Athumani Katimba, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha Tanzania inajenga uchumi wa viwanda, Serikali kupitia Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 imeweka mipango ya kuzalisha umeme wa kutosha na unaotabirika. Serikali kupitia Wizara ya Nishati imeweka mpango wa kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020. Kufutia mpango huo, Serikali inatekeleza miradi mbalimbali ya kuzalisha umeme kutokana na vyanzo mbalimbali vikiwemo maji, gesi asilia na jua. Miongoni mwa miradi ya kuzalisha umeme inayotekelezwa ni pamoja na upanuzi wa mradi wa kufua umeme kwa kutumia gesi asilia Kinyerezi I kutoka megawatts 150 za sasa na kufikia megawatts 335. Utekelezaji wake unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Agosti, 2019.

Mheshimiwa Spika, miradi mingine ya kufua umeme kwa gesi asilia ni Kinyerezi II, megawatts 240 ambao utekelezaji wake umekamilika mwezi Aprili, 2018, badala ya 2019 inayosomeka hapo na mradi wa kuzalisha umeme wa Mtwara wa megawatts 300 unaotekelezwa chini ya ufadhili wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Japan (JICA). Mradi huu unatarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Machi, 2019.

Mheshimiwa Spika, mwezi Disemba, 2018, Serikali ilianza kutekeleza mradi za kuzalisha umeme wa kutumia nguvu ya maji (Stiegler’s Gorge) megawatts 2,115 pamoja na mradi wa Rusumo, megawatts 80. Miradi mingine itakayoanza kutekelezwa hivi karibuni ni mradi wa Ruhudji, megawatts 358, mradi wa Rumakali, megawatts 222 na mradi wa Kakono, megawatts 87. Miradi hii inatarajiwa kukamilika ifikapo mwishoni mwa mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia itatekeleza miradi ya kuzalisha umeme wa nguvu za jua megawatts 150 (Kishapu), upepo megawatts 100 (Singida) na miradi ya Makaa ya Mawe megawatts 600.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa miradi hii itaongeza umeme katika gridi ya Taifa kutoka megawatts 1602 kutoka kwenye vyanzo vilivyotumika kuzalisha umeme kwa sasa na kufikia megawatts 10,000 ifikapo 2025.