Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 120 2019-04-23

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:-

Imekuwa ni kawaida sasa kwa Askari wa Usalama barabarani kusimamisha magari ya usafiri wa Umma kama vile daladala na mabasi na kadhalika:-

Je, ni lini Serikali itaandaa utaratibu wa kuwa na Vituo Maalum vya Ukaguzi huo ili kuokoa muda wa wasafiri?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rose Cyprian Tweve, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Usalama Barabani, Sura ya 168 iliyorejewa mwaka 2002 Kifungu cha 81, kinampa uwezo Askari Polisi wa kulisimamisha gari lolote barabarani au sehemu yoyote anapolitilia shaka na kulikagua au pindi linapokuwa limetenda kosa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani limeshaandaa utaratibu wa kuwa na vituo maalum vya ukaguzi wa mabasi ya Umma katika vituo vikuu vya mabasi vyote katika kila Mkoa ambapo mabasi ya abiria hufanyiwa ukaguzi kabla ya kuanza safari na pale yanapofika mwishoni wa safari.

Mheshimiwa Spika, aidha, ukaguzi wa pembezoni mwa barabara (road side inspection) ambao huhusisha mabasi ya daladala na vyombo vingine vya moto hufanyika katika vituo vya ukaguzi maalum (check points) ambavyo vipo katika barabara kuu na katika barabara nyingine za Miji pamoja na Majiji.