Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 95 2019-04-16

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:-

Kumekuwa na kilio cha uchakavu wa vituo vya polisi kwa upande wa Unguja na Pemba:-

(a) Je, ni vituo vingapi vipya vya polisi vilivyojengwa kwa upande wa Unguja na Pemba?

(b) Je, vituo hivyo vimejengwa na kampuni gani na ni vigezo gani vilivyoangaliwa katika ujenzi wa vituo hivyo?

(c) Je, ni lini Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara watafuatana nami kwenda kuviona vituo hivyo vilivyochakaa?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jaku Hashim Ayoub, Mbunge wa Baraza la Wawakilishi, lenye sehemu (a), (b) na (c), kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mikoa ya Unguja na Pemba vituo vingi vimejengwa au kukarabatiwa katika miaka tofauti, vikiwemo Vituo vya Mwembe Madafu na Mbweni katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Kituo cha Mchanga Mdogo Mkoani Kaskazini Pemba, Vituo vya Chwaka na Jambiani Mkoa wa Kusini Unguja na Vituo vya Chakechake na Mtambile Mkoa wa Kusini Pemba. Aidha, kuna ujenzi unaoendelea kwa sasa wa Vituo vya Chukwani, Dunga na Mkokotoni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, majengo mengi ya vituo hivi vya polisi ujenzi ulikuwa ni wa ushirikiano wa wananchi na Jeshi la Polisi. Hata hivyo, tunatambua mkandarasi aitwaye Albatina Construction Company Ltd anayejenga Kituo cha Polisi Mkokotoni ambaye kazi yake bado inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua kuwepo na uchakavu wa vituo vingi vya polisi katika Mikoa ya Unguja na Pemba kama vile vituo vya Mkoani Pemba, Kengeja, Micheweni, Konde, Mahonda, Nungwi, Kiwengwa na Kiboje ambapo hali ya kifedha ikiruhusu vitakarabatiwa. Viongozi wa Wizara wataambatana na Mheshimiwa Mbunge Jaku Hashim Ayoub tarehe 3/7/2019 kwenda kuviona vituo hivyo vilivyochakaa.