Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 10 Water and Irrigation Wizara ya Maji 86 2019-04-15

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. NAGU aliuliza:-

Maeneo mengi katika Wilaya ya Hanang’ yana matatizo ya maji ingawa Kata za Dirma, Lalaji, Wandela, Gawidu, Bassodesh na Mwanga zina visima vilivyochimbwa licha ya maji kutopatikana:-

Je, Serikali ina mikakati gani ya kutatua matatizo ya maji katika wilaya hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Michael Nagu, Mbunge wa Hanang’, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika juhudi za kutatua matatizo ya maji katika Wilaya ya Hanang’, Serikali inaendelea na utekelezaji wa miradi ya maji katika maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo katika Vijiji vya Hirbadaw, Kata ya Hirbadaw na Murumba, Kata ya Lalaji utekelezaji wa miradi upo katika hatua za mwisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Vijiji vya Bassodeshi, Nyabati, Gijetamuhog, Murumba, Gorimba, Diloda na Qalosendo katika Kitongoji cha Merekwa wananchi wanapata huduma ya maji kupitia visima vilivyochimbwa. Sehemu ya Kijiji cha Dirma iliyopo Kata ya Dirma inapata maji kutoka kwenye Mradi wa Maji ya Mtiririko wa Nangwa. Kijiji cha Gawidu ni miongoni mwa vijiji vitakavyojumuishwa katika miradi ya Bassotu ambapo utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 90. Aidha, utekelezaji wa mradi huo utaendelea katika vijiji vingine kwa awamu kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa Serikali ni kuendelea kutekeleza miradi mipya, kukamilisha inayoendelea na kukarabati ya zamani kwa kadri fedha zitakapopatikana ili kuhakikisha wananchi wa Wilaya ya Hanang’ wanapata huduma ya maji na yenye kutosheleza.