Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 70 2019-04-12

Name

Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. SAUL H. AMON) aliuliza:-

Hakuna barabara ya kuunganisha Daraja la Nyubati na Kata ya Kisondelea hadi Nzunyuke umbali wa zaidi ya kilomita 30 kufika kijiji cha Nyubati:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya kuunganisha Kijiji cha Nyubati na Kata ya Kisondelea?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saul Henry Amon, Mbunge wa Rungwe, kama ifuatavyo:-


Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa wananchi wamekuwa wakitembea umbali wa zaidi ya kilometa 30 kwa kuzunguka kutoka Nyubati hadi Nzunyuke kutokana na kukosekana kwa daraja. Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) umefanya usanifu na tathmini ya ujenzi wa barabara hiyo ambapo kiasi cha shilingi milioni 847.36 kinahitajika ili kuitengeneza barabara hiyo kwa kiwango cha changarawe. Katika mwaka wa fedha 2019/2020, TARURA imetenga kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Nyubati – Lutete yenye urefu wa kilometa 6 inayounganisha Kijiji cha Nyubati na Kata ya Kisondelea.