Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2019-04-12

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY atauliza:-

Serikali ina nia njema ya kuuweka Mji Mkongwe wa Mbulu kwenye mpango kabambe wa maboresho ya Miji na Majiji, Mikoa na Wilaya na kwenye Awamu ya Pili ya mpango huo kwa ajili ya miundombinu ya masoko, barabara, vituo vya mabasi na taa za barabarani:-

(a) Kwa kuwa Mji wa Mbulu ni mkongwe toka kuanzishwa kwake, je, ni lini sasa nia hiyo njema itatekelezwa?

(b) Je, mpango huo wa maboresho ya Mji utasaidiaje miundombinu ya barabara za mitaa ya Mji wa Mbulu ambazo ni zaidi ya kilomita 40 za changarawe kwa kuwa ni kilomita 1.8 za lami kwa sasa?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikalli kupitia Ofisi ya Rais - TAMISEMI inatekeleza miradi ya uboreshaji Miji Tanzania ambayo ni Urban Local Government Strengthening Programme (ULGSP) na Tanzania Strategic Cities Project (TSCP) na Dar es Salaam Metropolitan Development Project (DMDP) kwa fedha za mkopo nafuu toka Benki ya Dunia. Mpaka sasa miradi hii inatekelezwa katika Majiji 6, Manispaa 19 na Halmashaurui za Miji 6. Utekelezaji wa Programu ya Kuzijengea Uwezo Mamlaka za Miji (Urban Local Government Strengthening Programme-ULGSP) ulianza katika mwaka wa fedha 2013/2014 na unatarajiwa kukamilika mwaka wa fedha 2019/2020. Wakati wa maandalizi ya programu hii, Mji wa Mbulu ulikuwa haujapata hadhi ya kuwa Halmashauri ya Mji na hivyo kukosa vigezo vya kujumuishwa kwenye programu. Serikali itatoa kipaumbele kwa Mji wa Mbulu kwenye awamu nyingine za mradi huu.

(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, Programu ya Kuzijengea Uwezo Mamlaka za Miji inajumuisha ujenzi wa miundombinu ya msingi katika miji, kujenga uwezo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani na kuwezesha uandaaji wa mipango kabambe ya uendelezaji wa miji na kuboresha uwajibikaji na utawala bora. Hivyo Mji wa Mbulu ukijumuishwa utanufaika na mradi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inafahamu umuhimu wa kuboresha miundombinu ya barabara katika Mji wa Mbulu. Katika mwaka wa fedha 2018/2019 kupitia fedha za Mfuko wa Barabara, Serikali inajenga barabara yenye urefu wa kilomita 0.4 kwa kiwango cha lami nyepesi (double surface dressing) kwa gharama ya shilingi milioni 300 na kazi ya ujenzi inaendelea.