Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 8 Water and Irrigation Wizara ya Maji 64 2019-04-11

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:-

(a) Je, ni kwa nini Serikali imeshindwa kukamilisha mradi wa visima 23 ambavyo vingesaidia kama suluhisho la muda mfupi la tatizo la maji safi na salama katika Mji wa Tarime hususan kwenye maeneo ya Kata za pembezoni kama Nyandoto (Masurula), Nkende, Ketare, Kenyamanyori, Nyamisangura na Turwa?

(b) Mheshimiwa Rais alipofanya ziara Jimbo la Tarime Mjini Julai, 2018 aliwaeleza wananchi kuwa Serikali imetenga takriban shilingi bilioni 14 kwa ajili ya maji kutoka Ziwa Victoria ambayo itaondoa kabisa tatizo la maji katika Mji wa Tarime. Je, ni hatua gani imefikiwa kwenye ahadi hiyo hasa ikizingatiwa kuwa mradi huo upo kwenye mchakato kwa miaka mingi sasa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicolas Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Musoma (MUWASA) imeingia mkataba na Wakala wa Uchimbaji wa Visima na Ujenzi wa Mabwawa (DDCA) kwa ajili ya uchimbaji wa visima 23 katika Mji wa Tarime kwa gharama ya shilingi milioni 536.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa DDCA wanaendelea na utafiti wa maji chini ya ardhi (hydrological survey) na matarajio ya kazi ya uchimbaji wa visima hivyo itakamilika mwezi Septemba, 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utekelezaji wa ahadi ya Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa wananchi wa Tarime, Serikali imeshapata fedha kutoka Serikali ya India kiasi cha dola za Marekani milioni 500 kwa ajili ya uboreshaji wa huduma ya maji kwa miji 28 ya Tanzania Bara pamoja na Zanzibar ambapo Mji wa Tarime ni miongoni mwa Miji itakayopata maji kupitia fedha hizo. Kwa sasa taratibu za kuwapata wataalam washauri watakaofanya usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni unaendelea. Matarajio ya ujenzi wa miradi hiyo itaanza katika mwaka wa fedha 2019/2020.