Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 58 2019-04-10

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI (K.n.y. MHE. ENG. RAMO M. MAKANI) aliuliza:-

(a) Je, nini mpango wa Serikali kukamilisha mradi wa maji safi unaoendelea katika Mji wa Tunduru ili kuwaondolea wananchi hao adha kubwa wanayoipata ya uhaba wa huduma hiyo?

(b) Jimbo la Tunduru Kaskazini lina vijiji 92 ambapo taarifa za Serikali na takwimu zinaonesha kiwango cha upatikanaji wa maji kuwa chini sana:-

Je, ni lini mpango wa Serikali wa kuongeza kiwango hicho cha upatikanaji wa maji katika vijiji hivyo kufikia kiwango kilichowekwa kwa mujibu wa mipango ya Serikali na Ilani ya CCM itatekelezwa?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ramo Makani, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2016/2017 Mji wa Tunduru ulitengewa fedha kiasi cha shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya maji Mjini Tunduru na kuongeza hali ya upatikanaji wa maji. Uboreshaji huo ulisaidia kuongeza huduma ya maji kutoka asilimia 52 mwaka 2017 kufikia asilimia 66 kwa sasa. Aidha, kwa mwaka huu wa fedha 2018/2019, kupitia mamlaka ya majisafi na usafi wa mazingira Songea, inaendelea na utaratibu wa kutekeleza mradi wa upanuzi wa miundombinu ya maji kwa mji wa Tunduru ambapo wananchi wengi zaidi watapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Jimbo la Tunduru Kaskazini lina jumla ya vijiji 92 vyenye vituo vya kuchotea maji 385 vinavyohudumia wakazi wapatao 58,250. Katika kuhakikisha huduma ya maji safi na salama inaongezeka katika vijiji vilivyopo, Jimbo la Tunduru Kaskazini, Serikali inatekeleza miradi miwili ya Nandemo ambao umekamilika na mradi wa Matemanga ambao umefikia asilimia 85 ya utekelezaji na utahudumia vijiji vya Matemanga, Milonde, Changarawe na Jaribuni. Lengo la Serikali ni kuhakikisha huduma ya maji vijijini inafikia asilimia 85 ifikapo mwaka 2020 kama inavyoelekeza Ilani ya CCM.