Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 13 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 109 2016-05-05

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:-
Serikali imekuwa ikiendeleza zoezi la bomoa bomoa katika maeneo tofauti hapa nchini. Zoezi hili limekuwa likiwaathiri wananchi kiuchumi na hata kisaikolojia kwa kuwaacha wakiwa hawajui waelekee wapi:-
Je, kwa nini Serikali isiwafidie wananchi hawa ukizingatia kwamba wakati wanajenga, Serikali ilikuwa inawaona, lakini haikuchukua hatua stahiki?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali namba 109 la Mheshimiwa Juma Kombo Hamad, Mbunge wa Mwingwi, kama ifuatavyo:-
SPIKA: Wingwi. (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali namba 109, naomba kutoa maelezo yafuatayo:-
Mheshimiwa Spika, suala la bomoa bomoa katika maeneo tofauti hapa nchini limesababishwa na sababu zifuatazo:-
(1) Ni wananchi kuvamia kwenye maeneo hatarishi na oevu kinyume cha sheria;
(2) Ni kuvamia maeneo au viwanja vya watu wengine au maeneo ya wazi na ya umma bila kufuata utaratibu;
(3) Ni kujenga ndani ya hifadhi ya barabara, misitu, mbuga, mikoko, fukwe, kingo za bahari na mito; na
(4) Ni kujenga majengo kwenye maeneo yaliyopangwa bila kufuata taratibu.
Mheshimiwa Spika, mambo yote manne niliyotaja hapo juu na mengine yanayofanana na hayo yanasimamiwa na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 na Sheria ya Mipango Miji Na. 8 ya mwaka 2007.
Mheshimiwa Spika, bila kuathiri maana iliyopo katika Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya 2004, Kifungu cha 55 na 57 cha Sheria hii, vimeeleza wazi na kutoa katazo la kutoruhusu mtu yeyote kufanya shughuli zozote za kibinadamu za kudumu ndani ya mita 60 ambazo zinaharibu au kwa asili yake inaweza kuathiri ulinzi wa mazingira ya bahari au kingo za mito, mabwawa au miamba ya asili ya ziwa.
Aidha, Sheria hii pamoja na mambo mengine, imekataza shughuli zozote zinazohusisha kuchepusha au kuzuia mto, ukingo wa mto, ziwa au mwambao wa ziwa, ufukwe au ardhi oevu kutoka mkondo wake wa asili au kukausha mto au ziwa. Vile vile imeeleza wazi kuwa mtu yeyote anayekiuka masharti hayo anakuwa ametenda kosa.
Mheshimiwa Spika, pamoja na sheria tajwa hapo juu, Sheria ya Mipango Miji Na. 8 ya mwaka 2007 inaeleza na kufafanua kwa upana namna bora ya kusimamia ardhi yote ya Mijini kuwa, ―Sheria itaweka utaratibu wa maendelezo endelevu ya ardhi katika maeneo ya Mijini, kulinda na kuboresha huduma pamoja na kutoa vibali vya uendelezaji wa ardhi na kudhibiti matumizi ya ardhi katika masuala yanayohusiana na hayo.‖
Mheshimiwa Spika, wananchi wote watakaovunjiwa nyumba zao kwa sababu ya kutofuata sheria au kuvunja sheria au sababu nilizozitaja awali, hawatalipwa fidia.