Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 22 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 185 2016-05-18

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza:-
Kituo cha afya Kisesa kiliombewa kibali ili kipandishwe hadhi kuwa Hospitali kamili:-
Je, ni lini Serikali itatoa kibali?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa Sera ya Afya ya mwaka 2007, kila Wilaya inatakiwa kuwa na hospitali moja ya Wilaya na tayari hospitali hiyo ipo katika Wilaya ya Magu. Kituo cha Afya cha Kisesa kiliombewa kuboreshwa ili kiweze kutoa huduma za upasuaji mdogo kukidhi mahitaji hayo kwa wagonjwa badala ya kutegemea hospitali ya Wilaya pekee.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kituo hicho kianze kutoa huduma za upasuaji, Serikali iko katika hatua za mwisho za umaliziaji wa ujenzi wa jengo la upasuaji, jengo la kuhifadhia maiti pamoja na chumba cha X-ray. Aidha, tayari X-ray machine imeshapatikana, inasubiri tu kufungwa baada ya kukamilika kwa ujenzi wa chumba cha X-ray.