Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 42 2019-04-08

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL aliuliza:-

Je, ni lini wananchi wanaodai fidia ya maeneo yao yaliyopitiwa na mradi wa KV 400 katika Jimbo la Babati Mjini watalipwa.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Pauline Philip Gekul, Mbunge wa Babati Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 400 kutoka Singida hadi Namanga kupitia Arusha. Mradi huu unahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 400 yenye urefu wa kilomita 414 na upanuzi wa vituo vya kupozea umeme vya Singida na Arusha na usambazaji wa umeme katika vijiji 14 vinavyopitiwa na mradi. Gharama za mradi huu ni Dola za Kimarekani milioni 258.82.

Mheshimiwa Naibu Spika, ulipaji fidia ulianza mwezi Agosti, 2018 baada ya kukamilika kwa zoezi la uthamini na uhakiki wa mali na mazao yatakayoathirika na utekelezaji wa mradi. Hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi, 2019 fedha zaidi ya shilingi bilioni 31.87 zimeshalipwa kwa waathirika 2,815 kutoka Wilaya za Arusha, Monduri, Babati pamoja na Hanang’.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa Wilaya ya Babati, fedha zaidi ya shilingi 6,200,800,000 zimeshalipwa kwa wananchi 995 hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi, 2019. Wananchi 86 waliobaki watalipwa fedha zao shilingi milioni
638.18 wakati wowote baada ya kukamilika kwa zoezi la uhakiki linaloendelea.