Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 41 2019-04-08

Name

Prof. Norman Adamson Sigalla King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makete

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. PROF. NORMAN A. SIGALLA KING) aliuliza:-

Kumekuwa na maandalizi ya kuzalisha umeme katika Mto Lumakali uliopo Balogwa Makete na ni miaka 11 sasa wananchi wanaendelea kusubiri ambapo mwaka 2015/2016 Serikali ilitoa kauli kwamba ujenzi huo ungeanza mwaka 2017.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga bwawa hilo kwa ajili ya kuzalisha umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Norman Adamson Sigalla, Mbunge wa Makete kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mradi wa kuzalisha umeme katika mto Lumakali unahusisha ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme wa MW 222 na ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovoti 220 kutoka eneo patakapojengwa mitambo ya kuzalisha umeme Lumakali hadi Kituo cha Kupooza umeme cha Mbeya. Jumla ya gharama za mradi inakadiliwa kuwa Dola za Marekani milioni 388.22.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Lumakali ulifanyiwa upembuzi yakinifu mwaka 1998. Kwa sasa Mshauri Mwelekezi wa Mradi anakamilisha mapitio ili kuboresha Upembuzi Yakinifu uliofanyika mwaka 1998 na kazi hiyo itakamilika Mwezi Machi, 2020. Utekelezaji wa Mradi huu utaanza Mwezi Januari, 2021 na kukamlisha mwezi Juni, 2023.