Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 5 2019-04-02

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza:-

Je, Serikali iko tayari kubadilisha sheria/kanuni ili kuruhusu mazao ya misitu kusafishwa usiku na mchana (saa 24)?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato David Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Kuzuia Kusafirishwa kwa Mazao ya Misitu Na. 68 ya 2000, iliwekwa kutokana na changamoto za usafirishaji haramu wa mazao ya misitu ambapo kwa wakati huo ilikuwa ni vigumu sana kudhibiti uhalifu huo wakati wa usiku. Ukaguzi wa kina wa mazao ya misitu hufanyika kwenye kituo cha mwanzo cha safari na vituo vya ukaguzi vilivyoko barabarani kwa kukagua nyaraka mbalimbali ikiwa ni pamoja na kibali cha usafirishaji na kuangalia aina ya mazao, jamii ya miti na kiasi kinachosafirishwa. Kutokana na ugumu wa ukaguzi nyakati za usiku Serikali ilitunga Sheria ya Kuzuia Usafirishaji wa Mazao ya Misitu Nyakati za Usiku.

Mheshimiwa Spika, sababu nyingine iliyopelekea kuwepo kwa zuio la kusafirisha mazao ya misitu usiku wakati huo ni pamoja na uhaba wa watumishi, udanganyifu na ubadhirifu hali ambayo kwa sasa imeshughulikiwa. Hivyo, Wizara itaanza kutoa vibali maalum kwa wasafirishaji wa mazao ya misitu ya kupandwa kusafirishwa masaa 24. Mfano, mwaka 2018 kupitia Tangazo la Serikali Na. 478, Serikali imetoa kibali cha kusafirisha usiku nguzo za umeme kwa saa 24 ili kuharakisha usambazaji wa umeme vijijini.