Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 15 | Sitting 1 | Education, Science,Technology and Vocational Training, | Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi | 3 | 2019-04-02 |
Name
Susan Anselm Jerome Lyimo
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SUSAN A. J. LYIMO aliuliza:-
Je, ni fedha kiasi gani zilitumika kujenga mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yajulikanayo kama H.E Magufuli Hostel?
Name
William Tate Olenasha
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngorongoro
Answer
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Susan A. Lyimo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Spika, mradi wa ujenzi wa mabweni ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yajulikanayo kama Hostel za Dkt. J. P. J. Magufuli ulianza rasmi tarehe 1 Julai, 2016 na mabweni hayo yalikamilika na kukabidhiwa rasmi tarehe 15 Aprili, 2017. Ujenzi huo ulifanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kama Mkandarasi na kusimamiwa na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.
Mheshimiwa Spika, mradi huu uligharimiwa na Serikali kwa kiasi cha shilingi bilioni kumi tu.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved