Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 9 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 107 2019-02-07

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:-

Kwa muda mrefu kumekuwa na migogoro ya mipaka baina ya wananchi na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika maeneo ya Mkonkole Kata ya Tambuka Reli, Usule Kata ya Mbungani na Kata ya Cheyo Tabora Mjini:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kutatua mgogoro huo ambao ni wa muda mrefu?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Emanuel Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika Mji wa Tabora, JWTZ lina Kambi kwenye maeneo ya Airport, Cheyo, Bomani, Mirambo, Usule na Kalunde. Maeneo yote hayo yalipimwa na ramani zake kusajiliwa. Wakati wa upimaji maeneo mawili walikutwa watu wachache. Eneo la Airport alikutwa mwananchi mmoja aliyekuwa anaishi hapo. Mwananchi huyo alishafanyiwa uthamini na ameshalipwa fidia yake. Katika eneo la Usale zilikutwa familia tatu. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa limefanya mawasiliano na familia hizi kwa ajili ya kufanyiwa uthamini na hatua ya kulipwa fidia kwa kuzingatia upatikanaji wa fedha za maendeleo kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019.

Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuendeleza makazi katika Mji wa Tabora, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ilianza kupima viwanda ndani ya eneo la Kambi ya Mirambo ambalo tayari lilikuwa limepimwa. JWTZ ilichukua hatua ya kulifikisha suala hilo katika Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora ambayo ilisimamisha zoezi hilo. Wakati zoezi linasimamishwa, tayari wananchi wengine wameshagawiwa viwanja. Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa inaendelea kuwasiliana na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ili kuwaondoa wananchi hao ambao walipimiwa viwanja ndani ya eneo hilo likiwemo eneo la Tambuka Reli. Uondoshaji wa wananchi hawa utawezesha eneo hilo kuwa huu kwa matumizi ya kijeshi pekee.