Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 9 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 105 2019-02-07

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. KHATIB SAID HAJI aliuliza:-

FIFA inatoa misaada ya fedha kwa Tanzania kupitia TFF:-

Je, ni kiasi gani cha fedha TFF imekuwa ikiipatia Zanzibar kupitia ZFA?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khatib Said Haji, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli FIFA inatoa msaada wa fedha kwa mashirikisho ya mpira wa miguu ikiwepo TFF kwa ajili ya miradi na programu mbalimbali. Fedha hizo huwa ni maelekezo maalum kwa lengo la kusaidia na kuendeleza maeneo mahususi yafuatayo: Ligi ya Wanawake, ligi ya vijana, masuala ya kiutawala, kuinua vipaji kwa (Grassroot Program), Women’s Football Promotion, pamoja na Maendeleo ya Waamuzi.

Mheshimiwa Spika, kuanzia mwaka huu FIFA itakuwa inatoa jumla ya Dola za Kimarekani milioni 1.25 kila mwaka kwa wanachama wake wote ikiwepo ZFA, ambayo ni sehemu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania kwa mchanganuo ufuatao: fedha za miradi ya maendeleo kiasi cha Dola za Kimarekani 750,000, fedha kwa ajili ya kuendesha ofisi, Dola za Kimarekani 500,000.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa muda wa miaka mitatu sasa kutokana na kutokuwepo kwa uwazi katika matumizi ya fedha na kutokidhi vigezo vya utawala bora, TFF wamekuwa hawapati fedha hizo. Kazi kubwa imeshafanyika kurekebisha dosari zilizokuwepo za kiuhasibu na kiutawala bora. Hivyo, uwezekano ni mkubwa kwa TFF na ZFA kupokea fedha za msaada huo wa fedha mapema mwaka huu.