Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 9 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 101 2019-02-07

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-

Serikali imekuwa na utaratibu wa kukarabati shule zake za sekondari na za msingi nchini:-

Je, ni lini Serikali itafanyia ukarabati Shule za Sekondari Masagulu, Lwande, Mkuyu na Shule za Msingi Songe na Masagulu zilizopo Wilayani Kilindi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA C. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omary Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi ina jumla ya Shule za Msingi za Serikali 111 na Sekondari 22. Kuanzia mwaka 2015/2016 hadi 2017/2018 kupitia Mradi wa Lipa Kulingana na Matokeo (EP4R), Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi imepatiwa kiasi cha Sh.122,823,097 kwa ajili ya ujenzi na umaliziaji wa miundombinu ya shule za msingi na sekondari ambapo shule tatu za sekondari na 14 za msingi zimenufaika.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutekeleza programu mbalimbali za kuboresha miundombinu mashuleni ikiwemo ukarabati wa shule kongwe 89 nchini. Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi na wadau wengine wa maendeleo itaendelea kuweka kipaumbele cha ukarabati wa miundombinu ya shule ili kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunza. Aidha, natumia fursa hii kuzielekeza Halmashauri zote kutenga bajeti kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya shule.