Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 14 2018-11-07

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. GODFREY W. MGIMWA aliuliza:-
Wananchi wa Jimbo la Kalenga katika kata na vijiji mbalimbali wamejitolea kujenga miundombinu mbalimbali ikiwemo ujenzi wa zahanati na vituo vya afya lakini hakuna wauguzi na baadhi ya vifaa tiba. Je, Serikali inaisaidiaje Halmashauri kuhusu tatizo hilo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godfrey Mgimwa, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti,ili kutatua changamoto ya watumishi wa umma katika sekta ya afya, Serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada za afya kadri wanavyohitimu katika vyuo vya afya pamoja na hali ya bajeti inavyoruhusu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia Julai 2018/2019 Serikali imeajiri watumishi 8,447 wa kada mbalimbali za afya. Kati ya hao Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ilipangiwa watumishi 68 ambapo vituo vya kutolea huduma za afya vilivyoko katika Jimbo la Kalenga vilipata watumishi 40. Serikali inaendelea kutoa kipaumbele cha ajira kwa watumishi wa kada za afya ili kukabiliana na upungufu uliopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la vifaatiba, Halmashauri ya Wilaya ya Iringa inapokea fedha za Mfuko wa Pamoja wa Afya ambapo sehemu ya fedha hizo zinatumika kununulia vifaa tiba. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri ya Wilaya ya Iringa ilitumia shilingi 21,554,700 kwa ajili ya kununulia vifaa tiba ambavyo vilipelekwa katika vituo vya kutolea huduma za afya vilivyoko katika Jimbo la Kalenga. Vilevile Halmashauri inakusanya fedha za Mfuko wa Afya wa Jamii (CHF) ambazo kipaumbele cha matumizi kinapaswa kuwa ununuzi wa dawa na vifaa tiba.